Muigizaji Nyota wa Filamu za Kihindi, Sanjay Dutt kuitangaza Zanzibar kimataifa.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameupongeza ujio pamoja na azma ya Muigizaji Nyota wa Filamu za Kihindi, Sanjay Dutt ya kutaka kuekeza sambamba na kuwa Balozi wa kuitangaza Zanzibar kiutalii. Rais Dk. Mwinyi alitoa pongezi hizo Ikulu Jijini Zanzibar wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Muigizaji Nyota